Akizungumza na Mwanaroyal chuoni hapo Urafiki jijini Dar es salaam Mathayo alisema michezo hiyo itajumuisha Mpira wa miguu, Rede, na mpira wa kikapu michezo ambayo itampa fulsa ya kila mwanafunzi aweze kujijenga kiafya na kiakili pia.
Aidha aliongeza kua mchezo huo utakua wa kuwakalibisha wanafunzi wapya ambao ni wageni pamoja na wenyeji ambao watajenga timu ya kikosi cha Royal FC itayokua timu ya chuo.
Pia alisema kwa mujibu wa kocha wa kikosi wa timu hiyo Rajabu Mnakane ambaye ni kiongozi wa timu hiyo anatarajia kuona mchezo mzuri.
"Natoa wito kwa wanafunzi wanaoweza kucheza michezo niliyoitaja wajitokeze kwa wingi kujiandikisha pia siku ya ijumaa kwa wingi katika kukamilisha mchezo wa siku hiyo tuweze kupata timu ya Chuo,alisema Mathayo.
Hata hivyo Naibu waziri huyo alisema kutokana na kusua sua kwa michezo katika upande wa wasichana wizara hiyo imeongeza mchezo wa rede ili kuwawezesha kucheza michezo ambayo itawajengea ukakamavu.
"Pia napenda niwambie wanafunzi wasiangalie kipaumbele pia katika michezo sio katika masomo tu michezo ni sehemu ya elimu," alisema Mathayo.
Kwa upande wake msimamizi wa timu ya rede Elizabeth Joseph alisema baadhi ya wasichana wameanza kujitokeza na kusema kua mchezo huo utawajenga kiafya na kiakili kwa wanafunzi.
pia aliongeza kua mchezo wa rede unaweza kuchezwa na with hata wa 3 hivyo endapo watu hawatojitokeza kwa wingi unaweza kuchezwa na wachache kutokana na mchezo huo ulivyo
" wanafunzi wamejitoeza binafsi napenda rede nawasihii wanafunzi waje kujiandikisha kwa wingi ila endapo hawatojitokeza navyojua mchezo wa rede hata tukiwa watatu tunaweza kucheza,"alisema Joseph.
Aidha Joseph aliitaka serikali mpya ya wanafunzi kuboresha michezo mbalimbali chuoni. hapo hususa katika upande wa wasichana jambo ambalo limekua changamoto chuoni hapo katika serikali zilizopita.
Nae mmoja wa wanafunzi ambaye ni wa kitivo cha uwaandishi wa habari chuoni hapo Mwanahamis Mohamed amewaasa wanafunzi kujitokeza kwa wingi katika mchezo huo ili kufurahi pamoja
Pia alisema fulsa za michezo zimekua hazipatikani Mara kwa Mara katika vyuo vingi itachangia kujenga umoja na kusema kua wizara ya michezo imesikia kilio chao.
Mohammed alisema katika mchezo huo atashiriki vyema kabisa ambaye amejiandikisha katika mchezo huo na amejianda vyema katika mchezo wa rede.
" Nawashauri wasichana wenzangu wajitokeze kwa wingi kwa sababu fulsa kama hizi hua hazijitokezi Mara nyingi na waziri amesikia kilio cha wanafunzi cha muda mrefu," alisema Mohammed.
Mwanaroyal haikuishia apo ilizungumza na mmoja ya wachezaji katika upande wa miguu Johnson Johnson ambae ni mwanafunzi wa wa muhula wa mwisho ambaye aliipongeza wizara kwa kuliona jambo hilo.
Aisha Johnson aliwasihii wanafunzi wa muhula mpya kujitokeza kwa wingi katika mechi hiyo ili kuwajengea kujuana na kuweza kupata kikosi kimoja kwa ambacho kitakua kikiwakilisha Chuo katika michezo mbali mbali.
" Mi nawasihii wanafunzi waje kwa wingi katika huu mchezo na wachezaji wajitokeze tuweze kupata hamasa ya kucheza pambano ambalo tulikua tukisubiri kwa muda mrefu",alisema Johnson.
Hata hivyo Johnson aliishukuru serikali mpya kwa kuaanda michezo hiyo ambapo utawafanya wanafunzi kua na umoja na kuweza kushirikiana katika mbalimbali.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni